Plaza Premium Group strengthens Africa footprint with strategic entry into Tanzania
The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.
"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.
Vodacom Tanzania yazindua kampeni ya "Zaidi ya Mtandao", Ikiimarisha dhamira yake ya kuleta fursa zaidi ya huduma za mawasiliano
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.
“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima
Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.
“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.
PSSSF yatangaza fursa za uwekezaji kupitia Maonesho ya Nanenane
AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw. Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026
Sangu: PSSSF iwekeze fedha za wanachama kwenye miradi yenye tija
Ataka Uwekezaji wenye Tija
Na Mwandishi Wetu - Dar eÅ› Salaam
Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imeelekezwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali ili kuhakikisha mfuko unaendelea kuwa imara, endelevu na wenye uwezo wa kutoa huduma bora kwa wanachama.
Amesema hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Mfuko huo wa PSSSF iliyofanyika leo Agosti 1, 2026, PSSSF Commercial Complex, Jijini Dar es Salaam.
Aidha, Mhe. Sangu amesema jukumu kuu la bodi ni kusimamia shughuli za mfuko kama ilivyoainishwa katika Sheria ya PSSSF, kifungu cha 11 hususan katika maeneo makuu ya usimamizi ikiwemo huduma kwa wanachama, ukusanyaji wa michango, uwekezaji wa rasilimali za mfuko na ulipaji wa mafao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (Katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa PSSSF jijini Dar es Salaam Agosti 1, 2026
Vile vile, amesisitiza kuwa katika kutekeleza majukumu hayo, bodi inapaswa kuzingatia kikamilifu sheria, kanuni na miongozo ya Serikali pamoja na Mpango Mkakati wa PSSSF, ambao umeanza kutekelezwa pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Wajumbe mmeingia katika kipindi muhimu ambapo mfuko umeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano. Huu ndio utakaokuwa mwongozo wa utekelezaji wa majukumu na kufanikisha malengo ya mfuko,” amesema.
Kadhalika, amewataka wajumbe kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao, akibainisha kuwa Serikali ina matarajio makubwa kwa PSSSF katika kuhakikisha mfuko huo unakuwa imara.
Kuhusu uwekezaji, Waziri alisema fedha za wanachama zinapaswa kuwekezwa kwa umakini na weledi ili kulinda thamani yake na kuhakikisha zinazalisha faida itakayowezesha mfuko kutimiza wajibu wa kulipa mafao kwa wakati, hata baada ya miongo kadhaa.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo
“Fedha za wanachama zinawekwa leo kwa matarajio ya kulipa mafao miaka ijayo. Hivyo, ni muhimu ziwekezwe katika miradi yenye tija, salama na inayozingatia miongozo ya uwekezaji iliyowekwa na Serikali,” alisisitiza.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo
Mtendaji Mkuu WMA akutana na watumishi Arusha, asisitiza ufanisi

Watumishi wa Bunge wataka PSSSF kuendelea kubuni huduma
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’
Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu
Morogoro, Julai 31, 2026
Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.
Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.
“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.
Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.
Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.
![]() |
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro. |
Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine
Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati
“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.
Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.
Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
Jab yasimamia weledi na maadili ya uandishi wa habari

Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.
Dar yalipuka kwa hisani; Manyara yavuna shilingi 1.3 kuokoa watoto njiti

























































