Photo: Tanzania National Commission for UNESCO
Makonda Hatambui Jezi Mpya za Taifa Stars, Kamati Kuchunguza Mikataba
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Christian Makonda, ametangaza kutoutambua mchakato wa kubadilisha jezi za timu za taifa, akisema umefanyika bila kuishirikisha Wizara licha ya maelekezo aliyoyatoa Februari 2026.
Sambamba na hatua hiyo, Waziri Makonda ameagiza kuundwa kwa kamati maalumu itakayochunguza mikataba ya wazabuni wa jezi hizo, manufaa yake kwa timu za taifa pamoja na mapato yanayotokana na mauzo yake.
Uamuzi huo umetangazwa siku mbili baada ya Waziri Makonda kukataa hadharani jezi mpya zilizoonekana zikivaliwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, akisema hazikuwa na ubora unaoendana na hadhi ya Taifa Stars.
“Hii siyo jezi ya Taifa Stars. Taifa Stars kwa ubora wake hatuwezi kuwa na jezi za kiwango cha chini hivi. Acheni kutumia picha za Naibu wangu huku ofisi yangu haina taarifa. Tuheshimiane,” alisema Waziri Makonda kupitia mitandao ya kijamii.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara leo, Septemba 18, 2026, uchunguzi huo unalenga kubaini iwapo mikataba iliyopo inanufaisha timu za taifa kwa kiwango kinacholingana na fedha nyingi zinazotolewa na Serikali kugharamia timu hizo.
Wizara imeeleza kuwa Februari 2026, Waziri Makonda alitoa maelekezo ya kuboresha jezi za timu za taifa ili ziakisi utambulisho wa Tanzania na kuzalisha manufaa mapana kwa nchi.
Hatua hiyo imeelezwa kuwa muhimu kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika maandalizi ya timu za taifa zinazoshiriki mashindano ya kimataifa, pamoja na Tanzania kuwa mwenyeji mwenza wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027).
Kamati hiyo pia itachunguza mapato yanayotokana na mauzo ya jezi na mchango wake katika kugharamia uendeshaji wa timu za taifa.
Tanzania yasukuma matumizi yenye maadili na uwajibikaji ya akili unde


BRIDGE Tanzania Yawajengea Vijana Uwezo wa Kujitegemea

Young Innovators in Action as Msalato Girls Launch Technology Bootcamp
Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.

Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.

The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.
After the group discussions, the students came together for presentations.

Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.

Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.

It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.

Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.


TBN NA PSSSF WAJENGA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KUPANUA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII
Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) umeingia kwenye ushirikiano wa kimkakati na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa lengo la kutumia nguvu ya vyombo vya habari vya kidijitali kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, pensheni na uwekezaji.
Ushirikiano huo umejadiliwa wakati timu ya maofisa wa PSSSF ilipotembelea Makao Makuu ya TBN, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ambapo pande hizo zilikubaliana kushirikiana katika utoaji wa taarifa sahihi na uelimishaji wa umma kupitia majukwaa ya kidijitali.
Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alisema mtandao huo wenye zaidi ya wanachama 200 nchini na Diaspora una uwezo mkubwa wa kuifikisha elimu hiyo kwa wananchi kupitia majukwaa mbalimbali ya wanachama wake.
Msimbe alisema TBN iko tayari kutumia uzoefu na wigo wake kuwasaidia wananchi kuelewa huduma zinazotolewa na PSSSF, huku akisisitiza umuhimu wa wanachama wa mtandao huo kupata mafunzo ya kina kuhusu hifadhi ya jamii ili waweze kutoa taarifa sahihi na zenye tija.
Kwa upande wake, Mkuu wa Msafara wa PSSSF, Abdul Njaidi, alisema ushirikiano huo ni sehemu ya jitihada za mfuko kuwafikia wananchi kwa ufanisi zaidi kwa kushirikiana na wadau wa habari.
Njaidi alisema PSSSF itafanyia kazi mapendekezo yaliyowasilishwa na TBN, akisisitiza dhamira ya mfuko kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana kuhusu pensheni, hifadhi ya jamii na uwekezaji unaofanywa kwa manufaa ya wanachama na Taifa.
Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, alisema mtandao huo una uzoefu mkubwa katika habari za kidijitali na uko tayari kuwa kiungo kati ya PSSSF na wananchi.
“TBN ipo tayari kushirikiana na PSSSF kuhakikisha elimu ya hifadhi ya jamii inawafikia wananchi kwa lugha nyepesi, sahihi na inayoeleweka kupitia majukwaa ya kidijitali,” alisema Michuzi.
Ujumbe wa PSSSF uliongozwa na Abdul Njaidi na kuwajumuisha Regina Kumba, Grayson Mgunda na Doreen Lyimo, huku TBN ikiwasilishwa na Beda Msimbe, Rahel Pallangyo, Cathbert Kajuna na Issa Michuzi.
TANZANIA, ALGERIA KUSHIRIKIANA KUKUZA UZALISHAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA
MPOGOLO: MAFANIKIO YA WANAFUNZI NI MATUNDA YA KAZI ZA WALIMU

UNESCO CHAMPIONS DIGITAL SKILLS FOR TANZANIAN GIRLS

IFAD yaipongeza tanga kwa mafanikio ya AFDP

CRDB Bank na TRA SACCOS Wazindua TRA SACCOS PESACARD
Uzinduzi huo ni hatua muhimu katika ushirikiano wa muda mrefu kati ya Benki ya CRDB na TRA SACCOS, na unaashiria awamu mpya ya mageuzi ya kidijitali katika utoaji wa huduma za kifedha kwa wanachama wa SACCOS hiyo.
Kupitia TRA SACCOS PESACARD, wanachama wataunganishwa na mfumo mpana wa malipo wa Visa na hivyo kuwa na uwezo wa kutoa fedha kupitia ATM pamoja na kufanya malipo katika vituo vya POS vinavyokubali Visa ndani na nje ya Tanzania.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo aliipongeza TRA SACCOS kwa kufikisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake, huku akiipongeza Benki ya CRDB kwa kuendelea kutumia uwezo wake wa kiteknolojia na kifedha kusaidia taasisi mbalimbali kupanua huduma za kisasa za kifedha.
“Miaka 20 ni hatua kubwa inayodhihirisha uimara, uaminifu na mchango wa TRA SACCOS katika kuboresha ustawi wa kifedha wa wanachama wake. Nawapongeza viongozi na wanachama kwa kuendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati, na Benki ya CRDB kwa kutumia uwezo wake wa kifedha na kiteknolojia kujenga ushirikiano unaorahisisha upatikanaji wa huduma. Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD unaonesha mafanikio tunayoweza kuyapata pale taasisi za fedha na vyama vya ushirika vinapounganisha nguvu katika kukuza ubunifu na ujumuishi wa kifedha.”
Pamoja na uzinduzi wa kadi hiyo, ushirikiano huo umewezesha kuunganishwa moja kwa moja kwa mifumo ya TRA SACCOS na mifumo ya Benki ya CRDB. Maboresho hayo yanamaanisha kuwa mwanachama anaweza kutumia akaunti yake iliyopo ndani ya mfumo wa TRA SACCOS kupata huduma zinazohusiana na PESACARD bila kulazimika kuwa na akaunti katika benki nyingine ya biashara.
Muunganiko huo pia unatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa mikopo kwa wanachama. Fedha za mikopo zitaweza kutolewa moja kwa moja kupitia mfumo wa TRA SACCOS, hatua inayopunguza michakato ya kuhamisha fedha kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine na hivyo kupunguza muda wa mwanachama kusubiri fedha baada ya mkopo wake kuidhinishwa.
Katibu wa Benki ya CRDB, Pascal Mihayo, alisema hatua hiyo inaakisi dhamira ya Benki ya kutumia teknolojia na ushirikiano wa kimkakati kutengeneza suluhisho zinazojibu mahitaji halisi ya wateja.
“Kwetu Benki ya CRDB, huu ni zaidi ya uzinduzi wa kadi. Ni uthibitisho wa namna ushirikiano wa muda mrefu unavyoweza kukua na kuzaa suluhisho zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja. Kupitia TRA SACCOS PESACARD na muunganiko wa mifumo yetu, tunawapa wanachama uhuru zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, huku tukiiwezesha TRA SACCOS kuongeza kasi na ufanisi wa utoaji wa huduma. Haya ndiyo mageuzi ya kidigitali tunayoyasimamia, teknolojia inayorahisisha huduma, inayozisogeza karibu na wananchi na inayoongeza thamani halisi kwa mtumiaji.”
Miongoni mwa maboresho mengine muhimu ni kuunganishwa kwa huduma za TRA SACCOS na mtandao wa Mawakala wa CRDB. Hatua hiyo itawawezesha wanachama kuweka na kutoa fedha kupitia zaidi ya Mawakala 40,000 wa CRDB waliopo maeneo mbalimbali nchini, hivyo kupanua kwa kiasi kikubwa maeneo ambayo mwanachama anaweza kupata huduma.
Maboresho hayo yana umuhimu mkubwa hususan kwa wanachama waliopo nje ya maeneo yenye matawi ya benki, kwa kuwa yanapunguza utegemezi wa maeneo ya kawaida ya huduma za kifedha na kutumia mtandao mpana wa Benki ya CRDB kupeleka huduma karibu zaidi na mwanachama.
Kwa upande wake, Kamishnawa TRA, Yusuph Mwenda aliishukuru Benki ya CRDB kwa ushirikiano wake, akieleza kuwa PESACARD na muunganiko wa mifumo ni sehemu muhimu ya safari ya TRA SACCOS ya kuboresha na kufanya huduma zake kuwa za kisasa zaidi.
“Tunapoadhimisha miaka 20 ya TRA SACCOS, hatuangalii tu tulikotoka na mafanikio tuliyoyapata; tunaangalia pia tunakotaka kwenda na aina ya taasisi tunayotaka kuijenga kwa ajili ya wanachama wetu. TRA SACCOS PESACARD ni sehemu ya safari hiyo ya baadaye. Inawapa wanachama wetu urahisi, wigo mpana zaidi wa huduma na uwezo mkubwa wa kusimamia miamala yao. Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuamini maono yetu na kushirikiana nasi kuleta teknolojia inayoongeza uwezo wetu wa kuwahudumia wanachama vizuri zaidi.”
Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD pia unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara na taasisi za kifedha zinazomilikiwa na wanachama katika kuongeza ujumuishi wa kifedha. Kwa kuunganisha ukaribu wa TRA SACCOS na wanachama wake pamoja na teknolojia, miundombinu na uwezo wa malipo wa Benki ya CRDB, ushirikiano huo unalenga kuunda mazingira rahisi zaidi ya kupata huduma za kisasa za kifedha.
Kwa Benki ya CRDB, hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika teknolojia na kubuni suluhisho zinazoboresha uzoefu wa wateja na kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha. Benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na TRA SACCOS pamoja na taasisi nyingine katika sekta binafsi na umma kuleta mageuzi ya kidigitali na katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.




































