




Na Mwandishi Wetu, Kibaha
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameitaka Tanzania Biotech Production Ltd (TBPL) kuhakikisha inazingatia ubora katika uzalishaji wa mbolea hai ili kukidhi mahitaji ya soko na kulinda afya za watumiaji.
Kapinga alitoa kauli hiyo mjini Kibaha wakati wa hafla ya utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya TBPL, kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), na taasisi mbalimbali ikiwemo TFC, TARI, TFRA na TPHPA.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. .jpeg)


Na Mwandishi Wetu, Siha
Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro
inatarajiwa kupokea zaidi ya washiriki 800 kutoka ndani na nje ya
Tanzania katika mashindano makubwa ya michezo na utalii yajulikanayo
kama West Kili Forest Tour Challenge, yatakayofanyika Juni 20 hadi 21,
2026 katika ukanda wa msitu wa West Kilimanjaro.
Mashindano hayo
yamezinduliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Siha, Dkt. Christopher Timbuka,
aliyesema tukio hilo litakuwa chachu ya kuitangaza Siha kimataifa
kupitia utalii wa asili, michezo na shughuli za kijamii zitakazochochea
uchumi wa wananchi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt.
Timbuka alisema mashindano hayo yatahusisha mbio za kilomita 5, 10 na
21, pamoja na mashindano ya baiskeli na pikipiki yatakayopita katika
maeneo yenye mandhari ya kuvutia ya msitu wa West Kilimanjaro.
“Tunatarajia
kupokea washiriki wengi kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na nje ya
nchi. Hii ni fursa kubwa kwa Siha kuendelea kujitangaza kama kitovu cha
utalii wa michezo na uhifadhi wa mazingira,” alisema Dkt. Timbuka.
Aliongeza
kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika ili kuhakikisha mashindano
hayo yanafanyika kwa mafanikio makubwa huku yakitoa nafasi kwa wananchi
kunufaika kupitia biashara mbalimbali zikiwemo malazi, chakula, usafiri
na huduma nyingine za kijamii.
Kwa mujibu wa waandalizi, kabla ya
siku ya mashindano kutafanyika mkesha maalumu wa burudani
utakaojumuisha shughuli za kijamii, muziki, chakula na vinywaji kwa
washiriki na wadau mbalimbali.
Mashindano hayo yanaungwa mkono na
kampuni ya Mati Super Brands Ltd ambayo imeahidi kushirikiana
kuhakikisha tukio hilo linakuwa la kipekee na lenye mafanikio makubwa.
Akizungumza
kuhusu malengo ya mashindano hayo, Mratibu wa West Kili Forest Tour
Challenge, Bw. Mensier Elly, alisema tukio hilo si la michezo pekee bali
ni jukwaa muhimu la kutangaza vivutio vya utalii vya West Kilimanjaro
na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira kupitia michezo na utalii endelevu.
“Tunataka
kutumia michezo kama njia ya kuhamasisha jamii kuthamini mazingira na
wakati huo huo kuitangaza West Kilimanjaro kwa dunia,” alisema Bw. Elly.
Mashindano
hayo yanatarajiwa kuwa miongoni mwa matukio makubwa ya michezo na
utalii nchini mwaka huu kutokana na ushiriki mkubwa unaotarajiwa pamoja
na mvuto wa kipekee wa mazingira ya West Kilimanjaro.


Mbunge wa Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro, Dkt. Godwin Mollel akitoa neno.
Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti West Kilimanjaro, PCO Robert Faida akisoma risala.
Mratibu wa West Kili Forest Tour
Challenge, Bw. Mensier Elly
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM — Kampuni ya teknolojia ya kifedha ya Black Swan-Tanzania imeingia kwenye orodha ya kampuni 25 bora zinazochipukia barani Afrika kwa mwaka 2026 iliyotolewa na taasisi kubwa ya habari za fedha duniani, Bloomberg.
Black Swan, kampuni iliyosajiliwa Tanzania na inayojihusisha na huduma za kifedha kupitia teknolojia ya akili mnemba (AI), imetambuliwa kutokana na mchango wake wa kurahisisha upatikanaji wa mikopo nafuu na ya haki kwa Waafrika ambao bado hawajahudumiwa kikamilifu na mifumo rasmi ya kifedha.
Orodha hiyo ya Bloomberg hutambua kampuni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika zinazotatua changamoto muhimu kwa kutumia teknolojia na ubunifu wenye matokeo chanya katika jamii na uchumi.
Kupitia teknolojia yake, Black Swan hubadilisha taarifa za miamala ya kifedha inayofanyika kwenye simu za mkononi kuwa taarifa zinazoweza kusaidia taasisi za fedha kufanya tathmini sahihi za mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara wadogo ambao mara nyingi hawapo kwenye mfumo rasmi wa benki.
Akizungumzia mafanikio hayo, Mwanzilishi Mwenza na Afisa Mkuu Mtendaji wa Black Swan, Derick Kazimoto, alisema kutambuliwa huko ni ishara kuwa dunia inaanza kuona mchango wa kampuni hiyo katika kuboresha ujumuishaji wa kifedha barani Afrika.
“Tunafurahia kuona juhudi zetu zinatambulika kimataifa. Mamilioni ya Watanzania wanafanya kazi na biashara kila siku lakini bado hawaonekani katika mifumo rasmi ya fedha. Tuliianzisha Black Swan kubadilisha hali hiyo,” alisema Kazimoto.
Alisema teknolojia ya kampuni hiyo inachakata taarifa za kifedha kwa usalama na kwa idhini ya watumiaji ili kusaidia wakopeshaji kufanya maamuzi ya haraka, sahihi na yenye uwazi zaidi.
Kwa sasa Black Swan inahudumia zaidi ya taasisi 30 za kifedha Afrika Mashariki katika tathmini za mikopo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo mikopo midogo, mikopo ya kidijitali, ufadhili wa magari na mali nyingine pamoja na huduma za kawaida za mikopo.
Miongoni mwa bidhaa zake kuu ni “Kopa Gari”, mfumo wa kidijitali unaorahisisha upatikanaji wa mikopo ya magari ambapo majibu ya awali ya ustahiki wa mkopo hutolewa ndani ya dakika tano pekee.
Kampuni hiyo pia imeanzisha mfumo wa “Manka”, unaotumia akili mnemba kusaidia wakopeshaji kupata taarifa sahihi kuhusu uwezo wa mkopaji kulipa, hali inayosaidia kuongeza kasi na usahihi wa utoaji wa mikopo.
Kutambuliwa kwa Black Swan kunakuja wakati kampuni changa za teknolojia Afrika zikiendelea kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya bara hilo kutokana na mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa kidijitali.
Kupitia mafanikio hayo, Tanzania imeendelea kujijengea nafasi kwenye ramani ya ubunifu wa teknolojia Afrika sambamba na mataifa kama Nigeria, Kenya, Afrika Kusini na Morocco yaliyowakilishwa katika orodha hiyo ya Bloomberg.