Taifa Laomboleza: TRAMEPRO Yaungana na Waumini Kumkumbuka Kardinali Pengo


RC Rukwa Makongoro Nyerere Ampongeza Mwanae kwa Ushindi wa Mashindano ya Afrika Rally
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Makongoro Nyerere, amempongeza mwanawe Prince Nyerere pamoja na mjukuu wake Charles baada ya kutwaa tuzo ya ARC2 katika mashindano ya FIA African Rally Championship.
Kupitia ujumbe aliouchapisha mtandaoni, Nyerere alisema amefarijika na kujivunia mafanikio ya vijana hao, akieleza kuwa ni Watanzania wa kwanza kushinda tuzo hiyo katika zaidi ya miaka 45 ya mashindano hayo.

Aliongeza kuwa ushindi huo ni ushahidi kuwa nidhamu, bidii na uzalendo vinaweza kuzaa matokeo makubwa, huku akisisitiza kuwa mafanikio hayo yanaipa heshima familia na taifa kwa ujumla.

Vijana hao walitunukiwa tuzo hiyo Februari 15, 2026 katika hafla ya Tanzania National Motorsports Awards, hatua inayochukuliwa kama mafanikio makubwa kwa michezo ya magari nchini.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete aweka saini kitabu cha maombolezo cha Marehemu Kardinali Pengo
Serikali yaweka mkakati wa kuitangaza Tanzanite na madini ya vito nchini Qatar

Serikali ya Tanzania imeanza mkakati mpya wa kimataifa wa kutangaza madini ya Tanzanite katika soko la Mashariki ya Kati, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kurejesha hadhi na thamani ya madini hayo adimu duniani.
Akizungumza Februari 25, 2026 jijini Doha, Waziri wa Madini Anthony Mavunde alisema serikali imeamua kuongeza juhudi za kuitangaza Tanzanite kimataifa baada ya kubaini kuwa baadhi ya masoko bado hayafahamu asili ya madini hayo kuwa yanapatikana Tanzania pekee.
Aidha, serikali imepanga kuratibu ushiriki wa wafanyabiashara wa madini ya vito kutoka Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya madini yatakayofanyika Doha mwezi Aprili 2026, yakilenga kupanua masoko, kuongeza uwekezaji na kuimarisha utalii unaotokana na rasilimali madini.
Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mheshimiwa Habibu Awesi Mohamed, alisema fursa za ushirikiano katika sekta ya madini ni kubwa na zikiendelezwa zinaweza kuongeza mapato ya taifa na kukuza uchumi
Mapinduzi ya Malipo: Stanbic Bank Tanzania Yaleta Lipa Simpo Sokoni
Mkuu wa Idara ya Kidijitali na Biashara Mtandaoni Benki ya Stanbic Tanzania, Edward Balandya (watatu kushoto) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano, Dickson Senzi (wapili kushoto) wakiongea mfanyabiashara eneo la Mwenge wakati wa ziara ya kutembelea wafanyabishara na kuangalia jinsi ya kupokea malipo kupitia LIPA SIMPO ya benki hiyo na kusisitiza kasi, usalama na gharama nafuu ya suluhisho za malipo ya kidijitali za Stanbic kwa biashara za ndani.
Alisema kampeni za uhamasishaji zinazoendelea katika maeneo ya biashara nchini zinalenga kuonyesha matumizi halisi ya malipo kwa QR Code pamoja na kukusanya mrejesho kutoka kwa watumiaji wa huduma hiyo.
Kwa kuimarisha huduma za mawakala, malipo ya QR Code na gharama nafuu za miamala, Stanbic Bank Tanzania inaendelea kujiweka katika nafasi ya kuongoza mageuzi ya huduma za kifedha kidijitali nchini.
CRDB na Tume ya Madini Wapewa Sifa na Serikali kwa Mpango wa Kuinua Wachimbaji Wadogo
KAMPASI YA TPSC TABORA YATOA MISAADA NA KUFANYA USAFI - KITUO CHA WAZEE IPULI-TABORA

MAWAZIRI WAKUTANA MUHEZA KUTATUA MIGOGORO YA MASHAMBA YA UWEKEZAJI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe (Wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.





































