Royal Love Challenge 2026 Yatoa Washindi, Wajinyakulia Safari ya Valentine’s

Shinda Boda: PigaBet Yageuza Ushindi Kuwa Fursa ya Maisha
Dar es Salaam, Februari 10, 2026: Katika hatua inayoonesha mwelekeo mpya wa michezo ya kubahatisha nchini, PigaBet imezindua kampeni ya “SHINDA BODA” inayolenga si burudani pekee, bali pia kuwawezesha wachezaji—hasa vijana—kujipatia mtaji wa kujiajiri na kujiongezea kipato kupitia ushindi wa pikipiki mpya kila wiki.
Kampeni hiyo inawapa wachezaji wawili kila wiki fursa ya kushinda boda boda, zawadi ambayo kwa wengi imekuwa nyenzo muhimu ya kujiajiri au kuongeza kipato cha kila siku. Kupitia mfumo wa PigaPoints, kila mchezaji anayeshiriki michezo ya PigaBet ikiwemo Sports Betting, Casino na Aviator hujikusanyia pointi kwa kila bet au raundi, hali inayoongeza nafasi yake ya kuingia kwenye droo ya ushindi.
Akizungumza kuhusu dira ya kampeni hiyo, Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora, alisema kampeni ya Shinda Boda inalenga kuwafanya wachezaji waone thamani ya muda na ushiriki wao.
“Tumelenga kumwezesha mchezaji kubadili ushindi kuwa fursa ya maisha. Boda si zawadi tu, ni chombo cha ajira, ni mtaji na ni mwanzo wa safari ya kujitegemea kiuchumi,” alisema Kazola.
Tofauti na kampeni nyingi za awali, Shinda Boda imebuniwa kuunganisha burudani, ushindi na uwezeshaji wa kiuchumi. Wachezaji hawazuiliwi na mchezo mmoja pekee, bali wanaruhusiwa kucheza michezo mbalimbali ndani ya jukwaa la PigaBet, jambo linalowawezesha kukusanya pointi zaidi na kuongeza nafasi ya ushindi.
PigaBet pia imeendelea kuvutia wachezaji kwa promosheni zinazolinda na kuongeza thamani ya mchezaji, ikiwemo 10% Cashback kila Jumatatu kwa bet zilizopotea, Win Boost hadi 1000%, pamoja na huduma ya 2UP na Cashout, vinavyompa mchezaji udhibiti zaidi wa michezo yake.
Kwa kutambua nguvu ya mitandao ya kijamii, kampeni hiyo pia imefungua milango kwa content creators kupitia PigaBet Content Creator Challenge, itakayoratibiwa na mshirika wao WAKA.WIN. Kupitia mpango huo, wabunifu wa maudhui watapata nafasi ya kunufaika kifedha kwa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha kampeni.
Wadau wa michezo ya kubahatisha na vijana kwa ujumla wamehimizwa kujisajili kupitia www.pigabet.co.tz na kushiriki kampeni hiyo, huku PigaBet ikisisitiza umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
Kwa mtazamo mpya unaoangazia ajira na uwezeshaji, Shinda Boda imejipambanua kama kampeni inayotazama mbali zaidi ya ushindi wa muda mfupi, na kuweka msingi wa matumaini mapya kwa vijana wanaotafuta fursa za kujikwamua kiuchumi.
RC Sendiga Asisitiza Uwajibikaji na Kasi Utekelezaji wa Mradi wa REA Manyara

Naye mkandarasi aliyekabidhiwa utekelezaji wa mradi huo, Bw. Patrick Mong, amesema lengo lao ni kuukamilisha mradi huo ndani ya miezi 33, huku akibainisha kuwa kazi za utekelezaji zinaanza rasmi Februari 9 mwaka huu.Amesema mkandarasi amejiandaa kikamilifu kuhakikisha mradi unakamilika kwa ubora na kwa muda uliopangwa ili wananchi wa Mkoa wa Manyara wanufaike na huduma ya umeme kwa maendeleo endelevu.
BMT KUTEMBELEA KAMATI ZA MICHEZO ZA MIKOA 12 KUTATHMINI UTENDAJI

Akizungumza kuhusu mpango huo, Mkuu wa Kitengo cha Uendelezaji Michezo wa BMT, Bw. Benson Chacha, alisema ziara hiyo inalenga pia kuhakikisha kuwa Kamati za Michezo za Mikoa zinatimiza wajibu wao wa kusimamia na kuendeleza sekta ya michezo katika ngazi za mikoa.
Kwa mujibu wa Bw. Chacha, Kamati za Michezo za Mikoa hujumuisha Afisa Tawala wa Mkoa husika, Afisa Michezo wa Mkoa, Wajumbe saba walioteuliwa na Mkuu wa Mkoa, pamoja na mjumbe mmoja kutoka kila chama au shirikisho la michezo lililosajiliwa katika mkoa husika. Aidha, Maafisa Tawala wa Wilaya na Maafisa Michezo wa wilaya zote za mkoa husika ni wajumbe wa kamati hizo.
Alisema kamati hizo ndizo zenye jukumu la kutekeleza majukumu ya Baraza la Michezo la Taifa katika ngazi ya mikoa, ikiwamo usajili wa vyama na vilabu, usimamizi wa shughuli za michezo, uendelezaji wa vipaji, uimarishaji wa miundombinu ya michezo, pamoja na kuratibu mashindano mbalimbali.
Bw. Chacha alitaja mikoa itakayotembelewa kuwa ni Kagera, Shinyanga, Simiyu, Mara, Mwanza, Geita, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Singida na Tabora.
Aliongeza kuwa tathimini hiyo inalenga pia kupima utayari wa kamati hizo katika kuendeleza sekta ya michezo, ili kuchangia kuongeza ajira, kuimarisha amani na mshikamano wa jamii, kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika michezo, na kufikia matarajio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Tunataka kuona ni kwa namna gani Kamati za Michezo za Mikoa zimejipanga kuendesha michezo kwa kuzingatia misingi ya kitaifa, sambamba na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kupitia michezo,” alisema Bw. Chacha.
Aidha, alisema tathimini hiyo itaangalia hatua zilizochukuliwa na kamati hizo katika kuimarisha utawala bora, uwazi na uwajibikaji, hususan katika kusimamia shughuli za vyama na mashirikisho ya michezo ili viendeshwe kwa kuzingatia sheria na kanuni zilizopo.
Bw. Chacha alisisitiza kuwa BMT itaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wa michezo katika ngazi zote ili kuhakikisha sekta ya michezo nchini inaendelea kukua kwa tija na kuchangia maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
RC QUEEN SENDIGA AWASIHI WANAWAKE KUTAMBUA NAFASI ZAO NDANI YA NDOA, AONYA UKATILI WA KIJINSIA MANYARA
Manyara — Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, amewataka wanawake wakiwemo viongozi kutambua na kuheshimu nafasi zao ndani ya ndoa, akisisitiza kuwa mwanamke kufahamu haki zake hakumaanishi kumpunguzia heshima mumewe, kwani wanaume nao wanahitaji kutunzwa na kuheshimiwa.
“Wakina Mama amkeni na mfahamu nafasi na thamani zenu. Mwanamke kufahamu haki yako hakumaanishi usimuheshimu mumeo. Tukisimama hapa sisi ni viongozi, lakini tukirudi nyumbani sisi ni wake na mama wa familia, lazima tujue kucheza na nafasi hizo mbili,” alisema.Aidha, alionya tabia ya baadhi ya wanawake kujiona bora ndani ya nyumba hali inayochangia migogoro ya ndoa.
“Kuna wakati tunapata matatizo kwa sababu ya kujifanya tuna masharubu ndani. Ndani ya nyumba mwenye sharubu ni mmoja. Tunapodai haki zetu, basi na sisi tutimize wajibu wetu kama wake,” aliongeza.
RC Sendiga pia aliwakumbusha wanawake umuhimu wa malezi, usafi na mapenzi ndani ya familia, akisema kutokujali majukumu ya nyumbani kunasababisha migogoro na kuvuruga mahusiano.
“Akina Baba nao wana mioyo, wanahitaji kutunzwa. Ukisema huna muda wa kumtunza mume wala watoto, tutasaidiana vipi? Mahaba hayataki kelele, yanataka busara na upole,” alisema.

Kwa upande mwingine, aliwataka wanawake kuepuka tamaa ya fedha na miradi mingi isiyo na tija huku wakisahau majukumu ya msingi ya kifamilia, akisisitiza kuwa familia imara ni msingi wa jamii salama na taifa lenye maendeleo.
RC Sendiga alihitimisha kwa kutoa wito kwa viongozi wa jumuiya hiyo kuendelea kutoa elimu ya ndoa, malezi na maadili ili kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia na kujenga familia zenye mshikamano ndani ya Mkoa wa Manyara.
VALENTINE’S DAY YAJA NA MSISIMKO MPYA: MATI SUPER BRANDS LTD YAZINDUA ROYAL LOVE CHALLENGE 2026
Vodacom Tanzania Foundation Yaunga Mkono Afya ya Jamii Kupitia Kambi za Uchunguzi Bure
ZANZIBAR – Vodacom Tanzania Foundation imeanza rasmi utekelezaji wa kambi za afya bure Zanzibar kwa lengo la kusaidia jamii kupata uchunguzi wa mapema, elimu na huduma za kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza (NCDs), yakiwemo shinikizo la damu na kisukari, ambayo yameendelea kuwa changamoto kubwa kwa afya ya wananchi.
Takwimu zinaonesha kuwa takribani asilimia 34 ya magonjwa sugu nchini Tanzania yanahusishwa na magonjwa yasiyoambukiza, hali inayosababisha madhara makubwa kiafya endapo hayatagunduliki mapema. Zanzibar imekuwa miongoni mwa maeneo yenye ongezeko la wagonjwa wa shinikizo la damu na kisukari, hali iliyochochea haja ya kuimarisha jitihada za kinga na uchunguzi wa afya katika jamii.
Kambi ya afya inayofanyika kuanzia Februari 3 hadi 6, 2026 inalenga kutoa huduma za upimaji wa afya, ushauri wa kitaalamu na elimu kwa jamii kuhusu namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza. Uzinduzi rasmi wa kambi hiyo ulifanyika Februari 4, 2026, na kuhudhuriwa na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Msafiri Marijani.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Marijani alisema magonjwa ya shinikizo la damu na kisukari mara nyingi hayana dalili za awali, hivyo uchunguzi wa mapema ni muhimu katika kuzuia madhara makubwa ya kiafya. Alipongeza mchango wa Vodacom Tanzania Foundation katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha afya ya jamii kupitia mipango ya kinga na elimu.
Kwa upande wake, Meneja wa Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Sandra Oswald, alisema kambi hizo zimebuniwa mahsusi ili kupeleka huduma za afya moja kwa moja kwa wananchi, hususan wale wenye ufinyu wa upatikanaji wa huduma za uchunguzi wa mara kwa mara. Alisema kuanza kwa mpango huo Zanzibar ni hatua muhimu katika kupanua wigo wa huduma na kuongeza athari chanya kwa jamii.
Aliongeza kuwa Vodacom Tanzania Foundation itaendelea kushirikiana na wataalamu wa afya pamoja na wadau mbalimbali ili kuendeleza na kupanua mpango huo katika maeneo mengine ya nchi, ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika kufanikisha Lengo la Maendeleo Endelevu namba 3 (SDG 3) la Afya Njema na Ustawi.
Foundation hiyo imewahimiza wakazi wa Zanzibar kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kambi hizo za afya, ikisisitiza kuwa uchunguzi wa mapema, elimu na hatua za kinga ni msingi muhimu katika kujenga jamii yenye afya njema na ustawi endelevu.

CRDB Yaahidi Huduma za Kibenki Zinazomfuata Mteja Kupitia Kampeni Mpya 2026
FCC YAIMARISHA HUDUMA KWA WANANCHI KUPITIA MIFUMO YA KISASA
Tume ya Ushindani (FCC) imeweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa wakati kwa kutumia mifumo ya kisasa katika utekelezaji wa majukumu yake, ikiwa ni sehemu ya kuongeza ufanisi na uwazi katika huduma za ushindani na biashara nchini.
Akizungumza wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume hiyo kilicholenga kupanga mikakati ya utekelezaji wa majukumu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema hatua zinazochukuliwa na Tume zinalenga kuwahudumia wananchi kwa viwango vya juu vya ubora vinavyotambulika kitaifa na kimataifa.
Amesema FCC inaendelea kutekeleza dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha mazingira ya biashara nchini kwa kuwashirikisha wafanyabiashara na wananchi kupitia mifumo rafiki, ya kisasa na yenye ufanisi katika utoaji wa huduma.
Bi. Ngasongwa amebainisha kuwa katika kipindi cha siku 100 za uongozi wa Rais Samia, FCC imechukua hatua za makusudi za kusogeza huduma karibu na wananchi, ikiwemo kuanzisha Ofisi ya FCC Mkoa wa Tanga pamoja na maeneo ya mipakani, hatua iliyolenga kuongeza wigo wa huduma na kuwafikia wananchi waliopo maeneo ya pembezoni.
Ameongeza kuwa FCC imeendelea kudumisha Cheti cha Ithibati ya Ubora ISO 9001:2015 kutokana na jitihada zake za kutoa huduma kwa weledi, uwazi na kuzingatia viwango vya ubora, huku akiwapongeza watumishi kwa juhudi zao katika kulinda hadhi ya taasisi hiyo.
Katika kikao hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili na kutoa maoni kuhusu rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Tume wa miaka mitano (2026/27–2030/31), unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050, sambamba na kuimarisha utamaduni wa ushirikishwaji katika maamuzi ya taasisi.
Kikao kazi hicho cha FCC kimefanyika Februari 2, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond jijini Dar es Salaam.
Bw. Shalua Magandi, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi akichangia mada wakati wa kikao kazi na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.
Mwenyekiti wa Tughe Tawi la FCC, Bw. Emmanuel Ndyetabula akifuatilia kikao kazi cha Kaimu Mkurugenzi Mkuu na watumishi wa Tume, kilichofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tiffany Diamond, Jijini Dar es Salaam Februari 02,2026.






































.jpeg)