
Kampeni ya “KUTOA NI MOYO” yazinduliwa kwa kishindo


Na Mwandishi Wetu. Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Bw. Tido
Mhando, amewataka Waandishi wa Habari nchini kutafakari upya wajibu wao
katika kuijenga jamii kupitia maudhui yenye tija, akieleza kuwa ipo haja
ya kurejesha hadhi na nguvu ya taaluma hiyo katika kujenga fikra na
maendeleo ya taifa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Bw. Mhando
amesema pamoja na JAB kusimamia utoaji wa ithibati kwa kuzingatia vigezo
vya elimu na sheria, bado kuna umuhimu wa Waandishi wa Habari kuendelea
kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kitaaluma.
“Tukitazama baadhi
ya vyombo vyetu vya habari, iwe ni magazeti, redio au televisheni,
mambo ya kufikirisha kwa kiasi kikubwa yamepungua. Waandishi wa Habari
wanapaswa kutafakari kama hiyo ndiyo taswira wanayotaka kuiacha katika
jamii ya Watanzania,” amesema.
Amesisitiza kuwa vyombo vya habari
vina nafasi kubwa ya kuunda mtazamo wa jamii, hivyo kuna wajibu wa
kuhakikisha maudhui yanayotolewa yanajenga uelewa, yanakuza maendeleo na
yanalinda maslahi ya taifa.
“Tunachosimamia ni kuhakikisha
Mwandishi wa Habari anayepata ithibati anakuwa na kiwango cha elimu
kisichopungua Diploma, lakini tunataka pia Waandishi wa Habari waendelee
kupata mafunzo ili waweze kuimarika zaidi kitaaluma,” amesema.
Amesema
ipo haja ya sekta ya habari kutafakari aina ya maudhui yanayopewa
kipaumbele, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika
kujenga fikra na mwelekeo wa jamii.
Baada ya kupitia nyaraka zilizowasilishwa, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Babati, Ahmed Mgodo, alisema mahakama imejiridhisha kuwa Brayton Lucas ni mtoto na hivyo haina mamlaka ya kuendelea kusikiliza kesi hiyo. Kutokana na uamuzi huo, mahakama ilisimamisha shauri hilo dhidi ya mshtakiwa huyo na kuagiza polisi kuandaa hati mpya ya mashtaka kwa mujibu wa sheria zinazohusu watoto.
Brayton Lucas alipatiwa dhamana huku washtakiwa wawili wengine wakiendelea kushikiliwa. Wakili Thadei Lister amesema wako tayari kuendelea kumtetea mtoto huyo iwapo atafikishwa katika Mahakama ya Watoto.
MBUNGE
wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Mariam Ibrahim amemshuru Mwenyekiti wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa , Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa
kupendekeza jina lake na Kamati Kuu ya chama hicho kulipitisha na
hatimaye kushinda kwa kura nyingi.
Ametoa
shukrani hizo kwa Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Dk.Samia Suluhu Hassan
alipokuwa akisalimia viongozi mbalimbali wa Chama hicho wakati wa Semina
ya Uongozi na Maendeleo kwa madiwani wote wanawake wa Mkoa wa Pwani.
Ameyasema hayo leo alipokuwa mgeni rasmi katika mashindano ya “Mkali wa Chapati” yaliyofanyika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani ambapo amefafanua mashindano hayo ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha matumizi ya nishati safi chini ya uongozi wa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
Katika hatua nyingine, amewaomba wananchi wa wilaya hiyo kuendelea kushikamana na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa maendeleo ya jamii yao.
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhururi ya Muungano wa Tanzania imepanga kuajiri watumishi wapya 45,000 wa kada mbalimbali katika mwaka wa fedha 2026/27 ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha utumishi wa umma na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma nchini.
Mbali na ajira hizo mpya, Serikali pia imepanga kuwabadilishia muundo watumishi 5,865 pamoja na kuwapandisha madaraja watumishi 234,921.
Kauli hiyo imetolewa leo Mei 21, 2026 na Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha Menejimenti ya Waandishi Waendesha Ofisi (TAPSEA) uliofanyika Ngurdoto, jijini Arusha.
Aidha, amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira bora na wezeshi ya kazi kwa watumishi wa umma ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji kazi.
Amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2025/26 Serikali imeidhinisha ajira mpya za watumishi 42,500 wa kada mbalimbali, kupandisha vyeo watumishi 219,042, kuwabadilishia muundo watumishi 6,198 pamoja na kulipa malimbikizo ya mishahara kwa watumishi 18,083.
Katika hatua nyingine, Mhe. Ridhiwani amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa bidii na weledi huku akiwaasa waajiri kusimamia ipasavyo utendaji kazi wa watumishi ili kusaidia kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Na Jawadu Kinyobwa WAZIRI
wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Ridhiwani Kikwete amewataka wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa
viongozi waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuchangia maendeleo ya
jamii na taifa kwa ujumla.
Akizungumza Mei 15, 2026 katika
Mahafali ya Tisa ya Taasisi hiyo yaliyofanyika katika Mlimani City
jijini Dar es Salaam, Mhe. Ridhiwani alisema dunia ya sasa inahitaji
viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kufanya maamuzi kwa
kuzingatia maslahi ya wananchi.
Alisema uadilifu ni sifa muhimu
ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo wahitimu wanapaswa kutumia
maarifa na ujuzi walioupata kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwazi na
weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa viongozi wenye uzalendo. Tukumbuke msemo
wa wahenga kwamba adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti
mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za umma,”
alisema Ridhiwani.
Aidha, aliwataka wahitimu hao kulinda
rasilimali za taifa na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika maamuzi
yao ya kila siku ili kusaidia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi
nchini.
Alisema Tanzania inahitaji viongozi waaminifu na wenye
uwajibikaji ambao watatumia nafasi zao kuendeleza ustawi wa wananchi na
kuimarisha misingi ya utawala bora. 
Sambamba na hilo, Waziri
Ridhiwani alisema uongozi unaozingatia haki na uwazi utaendelea
kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya
nchi.
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu
wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo alisema taasisi hiyo imetimiza
miaka 15 tangu kuanzishwa kwake rasmi Julai mwaka 2010 kwa Hati ya Rais
kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu kwa ajili ya kujenga na
kuimarisha viongozi barani Afrika.
Alisema kwa kipindi hicho,
taasisi hiyo imefanikiwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi, kuandaa
mijadala ya kisera pamoja na kufanya tafiti na machapisho yaliyosaidia
kukuza maarifa ya kiuongozi.
Kwa upande wake, akizungumza kwa
niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed alisema mafunzo hayo
yamewajengea uwezo mkubwa wa kiuongozi na kuwasaidia kufanya maamuzi
yenye tija kwa taasisi na jamii.
Alisema mahafali hayo hayakuwa
tu hitimisho la mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko makubwa ya
kiuongozi na maendeleo binafsi waliyoyapata ndani ya miezi sita ya
programu hiyo.










