Afya kwa Wote Sasa Yatekelezwa: Serikali Yatenga Mabilioni Kuwahudumia Wasiojiweza

Na Mwandishi Wetu.
Katika hatua ya kuondoa mzigo wa gharama za matibabu kwa wananchi, Serikali imezindua utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote, utakaowezesha familia ya watu sita kupata huduma za afya 372 kwa gharama ya Sh 150,000 kwa mwaka.
Kwa mujibu wa Mratibu wa Elimu kwa Umma wa Mpango wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote, Said Makora, mpango huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi wote bila kujali uwezo wao wa kifedha.
Amesema kupitia mpango huo, huduma zitakazotolewa zinajumuisha uchunguzi wa maabara, radiolojia, dawa na vifaa tiba pamoja na upasuaji mdogo na mkubwa, kuanzia ngazi ya zahanati hadi hospitali za rufaa za taifa.
Makora alibainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeweka vyanzo maalum vya mapato vitakavyokusanya takribani Sh bilioni 201.9 katika mwaka wa fedha 2025/2026 ili kugharamia wananchi wasio na uwezo, huku zaidi ya Sh bilioni 48.2 zikiwa tayari zimekusanywa katika robo ya kwanza ambazo zitakazonufaisha kaya laki 276.
Aliongeza kuwa mpango huo pia unalenga kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika kwa kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto pamoja na kudhibiti magonjwa yanayoongoza kuathiri wananchi kama malaria, kifua kikuu na UKIMWI.
Kuhusu walengwa wa mpango huo, alisema tayari zaidi ya kaya 931,000 zimetambuliwa kupitia kanzidata ya TASAF, huku Serikali ikilenga kufikia zaidi ya kaya milioni 3.9 zitakazonufaika na mpango huo, gharama zao zikigharamiwa kikamilifu.
“Mpango huu unakwenda kubadili maisha ya wananchi kwa kuhakikisha wanapata huduma za afya kwa wakati bila hofu ya gharama,” alisema Makora.
Utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote unatarajiwa kuongeza usawa katika upatikanaji wa huduma za afya, kupunguza umasikini unaosababishwa na gharama za matibabu na kuimarisha ustawi wa jamii kwa ujumla.
Siku ya Maji Duniani 2026: TRAMEPRO Yatoa Wito wa Matumizi Sahihi ya Maji Tanzania
.jpeg)
WAKALA WA VIPIMO WATAKA WATANZANIA KUTUNZA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI

Mradi wa CERA Waimarisha Utafiti wa Mpunga, Watafiti Wapewa Mafunzo Maalum Tanzania
Mtafiti Mkuu wa mradi Prof. Suzana Nchimbi Msolla akizungumza na watafiti hao kabla ya kuanza zoezi hilo.
BILIONI 35 KUINUA UPATIKANAJI WA MAJI MKINGA, MRADI WAFIKIA 65%

VIJANA WANAGENZI KIGAMBONI WAANZA KUNG’ARA KATIKA MAKAMPUNI MAKUBWA NCHINI
.jpeg)

JAB: Uhuru wa Vyombo vya Habari Upo, Lakini Lazima Uendane na Maadili

Na Mwandishi Wetu.
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesisitiza kuwa uhuru wa vyombo vya habari nchini upo, unalindwa kisheria na unatambuliwa katika Katiba pamoja na Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, huku ikitoa wito kwa wanahabari kuzingatia maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kauli hiyo ya JAB imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Wakili Patrick Kipangula, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha moja kwa moja cha Hatua za Ushindi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Hope Channel Tanzania, leo Machi 17, 2026 jijini Dar es Salaam.
Ameeleza kuwa kifungu cha 7 cha Sheria ya Huduma za Habari kinaweka bayana haki na uhuru wa vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na haki ya mwandishi wa habari kutafuta, kuchakata na kusambaza taarifa, huku wananchi wakiwa na haki ya kupata taarifa sahihi kuhusu maendeleo yanayowazunguka.
“Uhuru wa vyombo vya habari upo na unalindwa kisheria. Mwandishi ana haki ya kutafuta na kusambaza taarifa, na mwananchi ana haki ya kupata taarifa. Huu ndio msingi wa uwazi na uwajibikaji katika jamii,” amesema Wakili Kipangula.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa uhuru huo unaambatana na wajibu wa kuzingatia maadili ya taaluma, akibainisha kuwa dhana ya uwajibikaji haipaswi kuchanganywa na kile kinachoitwa ukandamizaji wa vyombo vya habari.
Amebainisha kuwa baadhi ya malalamiko ya ukandamizaji yanatokana na kutokuzingatia misingi ya kitaaluma, hususan pale ambapo taarifa zinapotolewa bila uthibitisho, uwiano au kwa lugha isiyozingatia maadili.
“Ni muhimu kutofautisha kati ya uwajibikaji na ukandamizaji. Usipozingatia maadili ya taaluma, usiseme unakandamizwa. Uwajibikaji ni sehemu ya taaluma, na haupaswi kutafsiriwa kama kubanwa kwa uhuru wa habari,” amesisitiza Kipangula.
Katika hatua nyingine, Wakili Kipangula ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya sekta ya habari kupitia mageuzi ya kisheria na kisera, ikiwemo kufutwa kwa Sheria ya Magazeti iliyokuwa ikitajwa kuwa kandamizi na kuanzishwa kwa Sheria ya Huduma za Habari inayolenga kuimarisha uhuru, uwajibikaji na weledi katika tasnia hiyo.
Amesema maboresho hayo yameleta mwelekeo mpya unaowezesha vyombo vya habari na wanahabari kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi, huku wakizingatia viwango vinavyokubalika kitaaluma na kisheria.
Aidha, ametoa wito kwa wanahabari kuendelea kuilinda taaluma yao kwa kuzingatia ukweli, usahihi na uwiano katika utoaji wa taarifa, sambamba na kuheshimu haki za wananchi za kupata taarifa sahihi na kwa wakati kwa mujibu wa Sheria ya Kupata Taarifa.
Amesisitiza umuhimu kwa waajiri kote nchini kuhakikisha wanapata wataalamu wenye sifa stahiki kuingia katika menejimenti zao, sanjari na kuwatumia waandishi wenye ithibati, katika kazi zote za kihabari ili kulinda na kuipa thamani taaluma ya uandishi wa habari.
MAHAKAMA YATUPILIA MBALI SHAURI LA KUPINGA TUME YA UCHUNGUZI WA MATUKIO YA UVUNJIFU WA AMANI

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la mapitio lililofunguliwa kupinga uundwaji wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025.
Shauri hilo la Mapitio Namba 32537 la mwaka 2025 lilifunguliwa na Rosemary Mwakitwange pamoja na wenzake watatu dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wajumbe wa Tume hiyo ya Uchunguzi.
Katika maombi yao, walalamikaji waliiomba Mahakama Kuu ya Tanzania itoe amri ya kufuta uamuzi wa Samia Suluhu Hassan wa kuunda na kuteua wajumbe wa Tume hiyo tarehe 18 Novemba 2025, wakidai kuwa Rais alivuka mipaka ya mamlaka yake ya kisheria wakati wa kuunda chombo hicho.
Hata hivyo, baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Mahakama Kuu tarehe 13 Machi 2026 ilitupilia mbali shauri hilo, ikieleza kuwa Rais alitumia mamlaka yake kwa mujibu wa sheria wakati wa kuunda Tume hiyo.
Katika uamuzi wake, Mahakama ilieleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi, kifungu cha 3 kinampa Rais mamlaka ya kuunda Tume ya Uchunguzi na kuteua wajumbe wake.
Mahakama ilibainisha pia kuwa hakuna ushahidi uliowasilishwa unaoonesha kuwa Rais alivunja sheria au kwenda kinyume na matakwa ya sheria hiyo wakati wa kuunda Tume hiyo.
Aidha, Mahakama haikuona dalili ya upendeleo katika uteuzi wa wajumbe wa Tume, ikisisitiza kuwa sheria inampa Rais mamlaka ya kufanya uteuzi huo bila kuwekewa masharti ya ziada.
Kutokana na hoja hizo, Mahakama ilihitimisha kuwa maombi ya walalamikaji hayakuwa na msingi wa kisheria, hivyo ikaamua kuyatupilia mbali.
Shauri hilo liliendeshwa na jopo la mawakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, waliowakilisha Serikali katika shauri hilo.
Uamuzi huo unathibitisha uhalali wa kisheria wa uamuzi wa Rais wa kuunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyoripotiwa kutokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 nchini.


.jpeg)
.jpeg)





























.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

