
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na The Runners Club, imezindua rasmi mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zinazotarajiwa kufanyika Mei 17 mwaka huu jijini Dar es Salaam, huku zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakitarajiwa kushiriki.
Tukio hilo linalozidi kujizolea umaarufu kila mwaka, linalenga kuhamasisha mazoezi ya mwili, kukuza mshikamano wa kijamii pamoja na kuendeleza mtindo wa maisha yenye afya miongoni mwa Watanzania.
Kwa mujibu wa waandaaji, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na makundi matatu ya mbio ambayo ni kilomita 21.1 (Nusu Marathon), kilomita 10 na kilomita 5, yakitoa fursa kwa washiriki wa rika na viwango tofauti kushiriki.
Usajili wa kushiriki mbio hizo tayari umefunguliwa kupitia majukwaa rasmi, ambapo wakimbiaji wa kada zote, kuanzia wanariadha wakongwe hadi wapenda mazoezi na washiriki wa burudani, wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisema mbio hizo ni zaidi ya mashindano ya riadha, bali ni jukwaa muhimu la kuimarisha afya na ustawi wa jamii.
“Katika Absa, tunaamini katika kuleta athari chanya katika jamii tunazozihudumia. Absa Dar City Marathon siyo tu mbio, bali ni jukwaa linalokuza afya, umoja na ustawi wa jamii,” alisema Luhanga.
Aliongeza kuwa benki hiyo inajivunia kushirikiana na The Runners Club katika kuandaa tukio hilo na kuhimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki katika mazoezi ya mwili.
Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo na Makamu wa Rais wa The Runners Club, Godphrey Mindu, alisema marathon hiyo inaonesha ukuaji wa kasi wa utamaduni wa kukimbia nchini.
“Tumeshuhudia jamii zikikusanyika kupitia mazoezi ya viungo, na tukio hili ni sherehe ya mshikamano huo. Tunatarajia kuwapokea wakimbiaji wa viwango vyote na kuwapatia uzoefu bora siku ya mashindano,” alisema Mindu.
Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Felix Donald, alisema mbio hizo zina mchango mkubwa katika kukuza vipaji vya wanariadha chipukizi pamoja na kuimarisha nidhamu na afya kwa jamii.
“Matukio kama haya ni msingi wa kukuza riadha nchini. Tunayaunga mkono kwa sababu yanasaidia kujenga kizazi kipya cha wanamichezo,” alisema Donald.
Wawakilishi kutoka vilabu mbalimbali vya kukimbia walisisitiza kuwa tukio hilo limekuwa kiunganishi muhimu cha jamii. Johnson Mbunda “Balozi” kutoka Goba Roads Runners alisema marathon hiyo inawaunganisha wakimbiaji kutoka maeneo mbalimbali na kuwajengea urafiki wa kudumu.
Kwa upande wake, mwanachama wa Kigamboni Runners alisema tukio hilo limekuwa sehemu ya mkusanyiko wa kila mwaka unaowapa fursa washiriki kuungana na marafiki, familia pamoja na kukutana na watu wapya huku wakifurahia mandhari ya jiji la Dar es Salaam.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wanachama wa vilabu mbalimbali vya kukimbia ikiwemo Tabata Runners, TOT Runners, Absa Running Club, Salasala Runners na Kigamboni Runners, pamoja na wadhamini wa tukio hilo.
Ushiriki wao umeendelea kuonesha kukua kwa kasi kwa utamaduni wa kukimbia nchini na mshikamano mkubwa wa jamii katika kuunga mkono jitihada za kukuza afya kupitia michezo.
Benki ya Absa Tanzania kwa kushirikiana na The Runners Club, imezindua rasmi mbio za Absa Dar City Marathon 2026 zinazotarajiwa kufanyika Mei 17 mwaka huu jijini Dar es Salaam, huku zaidi ya washiriki 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakitarajiwa kushiriki.
Tukio hilo linalozidi kujizolea umaarufu kila mwaka, linalenga kuhamasisha mazoezi ya mwili, kukuza mshikamano wa kijamii pamoja na kuendeleza mtindo wa maisha yenye afya miongoni mwa Watanzania.
Kwa mujibu wa waandaaji, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na makundi matatu ya mbio ambayo ni kilomita 21.1 (Nusu Marathon), kilomita 10 na kilomita 5, yakitoa fursa kwa washiriki wa rika na viwango tofauti kushiriki.
Usajili wa kushiriki mbio hizo tayari umefunguliwa kupitia majukwaa rasmi, ambapo wakimbiaji wa kada zote, kuanzia wanariadha wakongwe hadi wapenda mazoezi na washiriki wa burudani, wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisema mbio hizo ni zaidi ya mashindano ya riadha, bali ni jukwaa muhimu la kuimarisha afya na ustawi wa jamii.
“Katika Absa, tunaamini katika kuleta athari chanya katika jamii tunazozihudumia. Absa Dar City Marathon siyo tu mbio, bali ni jukwaa linalokuza afya, umoja na ustawi wa jamii,” alisema Luhanga.
Aliongeza kuwa benki hiyo inajivunia kushirikiana na The Runners Club katika kuandaa tukio hilo na kuhimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki katika mazoezi ya mwili.
Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo na Makamu wa Rais wa The Runners Club, Godphrey Mindu, alisema marathon hiyo inaonesha ukuaji wa kasi wa utamaduni wa kukimbia nchini.
“Tumeshuhudia jamii zikikusanyika kupitia mazoezi ya viungo, na tukio hili ni sherehe ya mshikamano huo. Tunatarajia kuwapokea wakimbiaji wa viwango vyote na kuwapatia uzoefu bora siku ya mashindano,” alisema Mindu.
Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam, Felix Donald, alisema mbio hizo zina mchango mkubwa katika kukuza vipaji vya wanariadha chipukizi pamoja na kuimarisha nidhamu na afya kwa jamii.
“Matukio kama haya ni msingi wa kukuza riadha nchini. Tunayaunga mkono kwa sababu yanasaidia kujenga kizazi kipya cha wanamichezo,” alisema Donald.
Wawakilishi kutoka vilabu mbalimbali vya kukimbia walisisitiza kuwa tukio hilo limekuwa kiunganishi muhimu cha jamii. Johnson Mbunda “Balozi” kutoka Goba Roads Runners alisema marathon hiyo inawaunganisha wakimbiaji kutoka maeneo mbalimbali na kuwajengea urafiki wa kudumu.
Kwa upande wake, mwanachama wa Kigamboni Runners alisema tukio hilo limekuwa sehemu ya mkusanyiko wa kila mwaka unaowapa fursa washiriki kuungana na marafiki, familia pamoja na kukutana na watu wapya huku wakifurahia mandhari ya jiji la Dar es Salaam.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wanachama wa vilabu mbalimbali vya kukimbia ikiwemo Tabata Runners, TOT Runners, Absa Running Club, Salasala Runners na Kigamboni Runners, pamoja na wadhamini wa tukio hilo.
Ushiriki wao umeendelea kuonesha kukua kwa kasi kwa utamaduni wa kukimbia nchini na mshikamano mkubwa wa jamii katika kuunga mkono jitihada za kukuza afya kupitia michezo.









.jpeg)















.jpeg)
















