
KAMPASI YA TPSC TABORA YATOA MISAADA NA KUFANYA USAFI - KITUO CHA WAZEE IPULI-TABORA



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe (Wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (wapili kushoto) akiwasili katika katika hafla ya uzinduzi wa programu ya Go Green Na IMBEJU inayolenga kuwezesha biashara na bunifu za kijani za vijana kama sehemu ya kuchochea uchumi wa kijani kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Alioongozana nao ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa.
Dar es Salaam, Februari 10, 2026: Katika hatua inayoonesha mwelekeo mpya wa michezo ya kubahatisha nchini, PigaBet imezindua kampeni ya “SHINDA BODA” inayolenga si burudani pekee, bali pia kuwawezesha wachezaji—hasa vijana—kujipatia mtaji wa kujiajiri na kujiongezea kipato kupitia ushindi wa pikipiki mpya kila wiki.
Kampeni hiyo inawapa wachezaji wawili kila wiki fursa ya kushinda boda boda, zawadi ambayo kwa wengi imekuwa nyenzo muhimu ya kujiajiri au kuongeza kipato cha kila siku. Kupitia mfumo wa PigaPoints, kila mchezaji anayeshiriki michezo ya PigaBet ikiwemo Sports Betting, Casino na Aviator hujikusanyia pointi kwa kila bet au raundi, hali inayoongeza nafasi yake ya kuingia kwenye droo ya ushindi.
Akizungumza kuhusu dira ya kampeni hiyo, Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora, alisema kampeni ya Shinda Boda inalenga kuwafanya wachezaji waone thamani ya muda na ushiriki wao.
“Tumelenga kumwezesha mchezaji kubadili ushindi kuwa fursa ya maisha. Boda si zawadi tu, ni chombo cha ajira, ni mtaji na ni mwanzo wa safari ya kujitegemea kiuchumi,” alisema Kazola.
Tofauti na kampeni nyingi za awali, Shinda Boda imebuniwa kuunganisha burudani, ushindi na uwezeshaji wa kiuchumi. Wachezaji hawazuiliwi na mchezo mmoja pekee, bali wanaruhusiwa kucheza michezo mbalimbali ndani ya jukwaa la PigaBet, jambo linalowawezesha kukusanya pointi zaidi na kuongeza nafasi ya ushindi.
PigaBet pia imeendelea kuvutia wachezaji kwa promosheni zinazolinda na kuongeza thamani ya mchezaji, ikiwemo 10% Cashback kila Jumatatu kwa bet zilizopotea, Win Boost hadi 1000%, pamoja na huduma ya 2UP na Cashout, vinavyompa mchezaji udhibiti zaidi wa michezo yake.
Kwa kutambua nguvu ya mitandao ya kijamii, kampeni hiyo pia imefungua milango kwa content creators kupitia PigaBet Content Creator Challenge, itakayoratibiwa na mshirika wao WAKA.WIN. Kupitia mpango huo, wabunifu wa maudhui watapata nafasi ya kunufaika kifedha kwa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha kampeni.
Wadau wa michezo ya kubahatisha na vijana kwa ujumla wamehimizwa kujisajili kupitia www.pigabet.co.tz na kushiriki kampeni hiyo, huku PigaBet ikisisitiza umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
Kwa mtazamo mpya unaoangazia ajira na uwezeshaji, Shinda Boda imejipambanua kama kampeni inayotazama mbali zaidi ya ushindi wa muda mfupi, na kuweka msingi wa matumaini mapya kwa vijana wanaotafuta fursa za kujikwamua kiuchumi.

Naye mkandarasi aliyekabidhiwa utekelezaji wa mradi huo, Bw. Patrick Mong, amesema lengo lao ni kuukamilisha mradi huo ndani ya miezi 33, huku akibainisha kuwa kazi za utekelezaji zinaanza rasmi Februari 9 mwaka huu.Amesema mkandarasi amejiandaa kikamilifu kuhakikisha mradi unakamilika kwa ubora na kwa muda uliopangwa ili wananchi wa Mkoa wa Manyara wanufaike na huduma ya umeme kwa maendeleo endelevu.

Akizungumza kuhusu mpango huo, Mkuu wa Kitengo cha Uendelezaji Michezo wa BMT, Bw. Benson Chacha, alisema ziara hiyo inalenga pia kuhakikisha kuwa Kamati za Michezo za Mikoa zinatimiza wajibu wao wa kusimamia na kuendeleza sekta ya michezo katika ngazi za mikoa.
Kwa mujibu wa Bw. Chacha, Kamati za Michezo za Mikoa hujumuisha Afisa Tawala wa Mkoa husika, Afisa Michezo wa Mkoa, Wajumbe saba walioteuliwa na Mkuu wa Mkoa, pamoja na mjumbe mmoja kutoka kila chama au shirikisho la michezo lililosajiliwa katika mkoa husika. Aidha, Maafisa Tawala wa Wilaya na Maafisa Michezo wa wilaya zote za mkoa husika ni wajumbe wa kamati hizo.
Alisema kamati hizo ndizo zenye jukumu la kutekeleza majukumu ya Baraza la Michezo la Taifa katika ngazi ya mikoa, ikiwamo usajili wa vyama na vilabu, usimamizi wa shughuli za michezo, uendelezaji wa vipaji, uimarishaji wa miundombinu ya michezo, pamoja na kuratibu mashindano mbalimbali.
Bw. Chacha alitaja mikoa itakayotembelewa kuwa ni Kagera, Shinyanga, Simiyu, Mara, Mwanza, Geita, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Singida na Tabora.
Aliongeza kuwa tathimini hiyo inalenga pia kupima utayari wa kamati hizo katika kuendeleza sekta ya michezo, ili kuchangia kuongeza ajira, kuimarisha amani na mshikamano wa jamii, kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika michezo, na kufikia matarajio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Tunataka kuona ni kwa namna gani Kamati za Michezo za Mikoa zimejipanga kuendesha michezo kwa kuzingatia misingi ya kitaifa, sambamba na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kupitia michezo,” alisema Bw. Chacha.
Aidha, alisema tathimini hiyo itaangalia hatua zilizochukuliwa na kamati hizo katika kuimarisha utawala bora, uwazi na uwajibikaji, hususan katika kusimamia shughuli za vyama na mashirikisho ya michezo ili viendeshwe kwa kuzingatia sheria na kanuni zilizopo.
Bw. Chacha alisisitiza kuwa BMT itaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wa michezo katika ngazi zote ili kuhakikisha sekta ya michezo nchini inaendelea kukua kwa tija na kuchangia maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Manyara — Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, amewataka wanawake wakiwemo viongozi kutambua na kuheshimu nafasi zao ndani ya ndoa, akisisitiza kuwa mwanamke kufahamu haki zake hakumaanishi kumpunguzia heshima mumewe, kwani wanaume nao wanahitaji kutunzwa na kuheshimiwa.
“Wakina Mama amkeni na mfahamu nafasi na thamani zenu. Mwanamke kufahamu haki yako hakumaanishi usimuheshimu mumeo. Tukisimama hapa sisi ni viongozi, lakini tukirudi nyumbani sisi ni wake na mama wa familia, lazima tujue kucheza na nafasi hizo mbili,” alisema.Aidha, alionya tabia ya baadhi ya wanawake kujiona bora ndani ya nyumba hali inayochangia migogoro ya ndoa.
“Kuna wakati tunapata matatizo kwa sababu ya kujifanya tuna masharubu ndani. Ndani ya nyumba mwenye sharubu ni mmoja. Tunapodai haki zetu, basi na sisi tutimize wajibu wetu kama wake,” aliongeza.
RC Sendiga pia aliwakumbusha wanawake umuhimu wa malezi, usafi na mapenzi ndani ya familia, akisema kutokujali majukumu ya nyumbani kunasababisha migogoro na kuvuruga mahusiano.
“Akina Baba nao wana mioyo, wanahitaji kutunzwa. Ukisema huna muda wa kumtunza mume wala watoto, tutasaidiana vipi? Mahaba hayataki kelele, yanataka busara na upole,” alisema.

Kwa upande mwingine, aliwataka wanawake kuepuka tamaa ya fedha na miradi mingi isiyo na tija huku wakisahau majukumu ya msingi ya kifamilia, akisisitiza kuwa familia imara ni msingi wa jamii salama na taifa lenye maendeleo.
RC Sendiga alihitimisha kwa kutoa wito kwa viongozi wa jumuiya hiyo kuendelea kutoa elimu ya ndoa, malezi na maadili ili kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia na kujenga familia zenye mshikamano ndani ya Mkoa wa Manyara.