Na Mwandishi Wetu.
“Tuendelee kumuombea Mheshimiwa Rais wetu awe na afya njema ili aendelee kuiongoza nchi kwa hekima na mafanikio,” ameongeza.

Na Mwandishi Wetu.
“Tuendelee kumuombea Mheshimiwa Rais wetu awe na afya njema ili aendelee kuiongoza nchi kwa hekima na mafanikio,” ameongeza.


Na Ruth Kyelula, Manyara
Mkoa wa Manyara unatarajia kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kimkoa tarehe 8 Machi 2026 katika Wilaya ya Simanjiro, huku Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Queen Sendiga, akitoa wito kwa jamii kuhakikisha haki za wanawake na wasichana zinalindwa na kuheshimiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari Machi 3, 2026 ofisini kwake mjini Babati, Sendiga alisema maadhimisho hayo ni fursa muhimu ya kuhamasisha jamii kushiriki katika juhudi za kukuza usawa wa kijinsia, kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuimarisha ustawi wao katika jamii.
Alisema Mkoa wa Manyara umekuwa ukikabiliwa na changamoto ya matukio ya ukatili wa kijinsia, lakini juhudi mbalimbali zimeendelea kufanyika ili kukabiliana na tatizo hilo. Alisisitiza kuwa wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuhakikisha watoto, hususan wasichana, wanapata haki zao na kulindwa dhidi ya vitendo vya ukatili.
Sendiga alieleza kuwa chimbuko la Siku ya Wanawake Duniani linatokana na harakati za wanawake wafanyakazi waliopigania haki zao kazini, jambo linaloifanya siku hiyo kuwa jukwaa la kuhimiza uwajibikaji kwa wanawake pamoja na kuwakumbusha waajiri, taasisi na serikali kuhakikisha mazingira ya kazi yanazingatia usawa wa mishahara, maslahi na fursa.
Aliongeza kuwa Tanzania imekuwa ikiadhimisha siku hiyo tangu mwaka 1997 kwa lengo la kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa ni “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050.”


Kwa niaba ya Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO), tunaungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Tanzania Wildlife Management Authority (TAWA), pamoja na wadau wote wa uhifadhi wa mazingira, vyombo vya habari, na watabibu asili nchini kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanyamapori tarehe 03 Machi 2026. Aidha, tunaungana na mataifa mengine duniani kusherehekea siku hii muhimu inayotukumbusha wajibu wetu wa kulinda urithi wa asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Maadhimisho ya mwaka huu yanatukumbusha umuhimu wa kulinda na kutumia kwa busara rasilimali za asili, hususan mimea ya dawa na harufu, ambayo imekuwa nguzo muhimu katika afya ya jamii, ukuaji wa uchumi wa taifa, na ustawi wa binadamu kwa ujumla. Mimea hii si tu hazina ya tiba asilia bali pia ni rasilimali yenye mchango mkubwa katika tafiti za kisayansi, viwanda vya dawa, na maendeleo ya kijamii.
Tanzania imebarikiwa kuwa na bioanuwai adhimu ya wanyamapori, misitu, na vyanzo vya maji. Rasilimali hizi ni urithi wa taifa letu na msingi wa maendeleo endelevu. Hivyo basi, tunapaswa kushirikiana kwa dhati katika:
• Kulinda wanyamapori dhidi ya ujangili na uharibifu wa makazi yao.
• Kuhifadhi mimea ya tiba kwa matumizi endelevu yasiyoharibu mazingira.
• Kulinda vyanzo vya maji na mifumo ya ikolojia kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.
• Kuwezesha jamii kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi na kunufaika nazo kiuchumi.
Tukiongozwa na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025–2050 inayolenga kujenga taifa lenye uchumi imara, amani, utulivu na maendeleo endelevu ya watu wake, tunasisitiza kuwa:
“Uhifadhi wa rasilimali za asili ni msingi wa ustawi wa taifa na kizazi kijacho.”
Kwa pamoja, tushikamane kulinda urithi wetu wa asili, kuenzi thamani ya mimea ya dawa, na kuhakikisha matumizi yake yanafanyika kwa njia endelevu kwa manufaa ya binadamu na mazingira.
TUSHIRIKIANE KWA UHIFADHI, USTAWI NA MAENDELEO ENDELEVU
Imetolewa na: Boniventura Mwalongo
Katibu Mkuu Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO).


Na Mwandishi Wetu.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, leo Machi 4, 2026, ametembelea Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) jijini Dar es Salaam ambapo amekukutana na watumishi na kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.
Akizungumza katika kikao na watumishi hao, Mhe. Mwinjuma alisisitiza umuhimu wa Bodi kusimamia sheria kikamilifu bila kupepesa, kuhakikisha kanuni zinaimarishwa, kufuatilia na kudhibiti wanaofanya kazi za habari bila ithibati ili kulinda hadhi ya taaluma.


Mhe. Mwinjuma amepongeza juhudi za Bodi katika kusimamia utekelezaji wa Sheria hadi sasa, huku akisisitiza kuwa haupaswi kulegalega ili kuimarisha weledi, uwajibikaji na imani ya umma kwa vyombo vya habari nchini.
Katika ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, pamoja na kuelezea utekelezaji wa majukumu, amefafanua mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja tangu kuzinduliwa kwa bodi ikiwemo uanzishaji wa mifumo ya usajili wa Waandishi, utoaji wa Ithibati na Vitambulisho vya Uandishi (Press Cards), utoaji wa elimu kwa umma, usimamizi wa maadili ya taaluma na uandaaji wa nyaraka zote muhimu za uanzishwaji wa Taasisi chini ya Msajili wa Hazina.
Aidha, kikao kilijadili changamoto zinazoikabili sekta ya habari, hususan uzingatiaji wa maadili katika vyombo vya habari vya mtandaoni na uhitaji wa rasilimali zaidi.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Milki Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Upendo Matotola akimkabidhi mwanamama mkazi wa jiji la Dar es Salaam Hati Milki ya ardhi katika Samia Ardhi Kliniki inayoendelea jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA, MICHUZI TV).
RUVUMA, Februari 28, 2026 — Katibu Mkuu wa TRAMEPRO, Boniventura Mwalongo, ametoa wito kwa Watanzania kugeuza historia ya mashujaa wa Vita vya Maji Maji kuwa chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi badala ya kubaki katika kumbukumbu pekee.
Mwalongo alisisitiza kuwa maadhimisho hayo yanapaswa kuwa jukwaa la kuhamasisha uwekezaji katika utalii wa kihistoria, tafiti za kisayansi pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuhifadhi makumbusho na nyaraka muhimu za historia. Aliongeza kuwa maeneo ya kihistoria yanaweza kuboreshwa na kuwa vivutio vya utalii, hatua itakayosaidia kufungua ajira kwa vijana na kuimarisha uchumi wa maeneo husika..jpeg)
Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Lucy Kabyemera, amesema kliniki hiyo itaendeshwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi za Ardhi za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.