Na Mwandishi Wetu

Na Mwandishi Wetu


Na Mwandishi Wetu, Arusha.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetumia Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu-KiliFair 2026 kutangaza mafanikio ya mpango wa bima ya lazima kwa wasafiri, ikieleza kuwa umeimarisha usalama wa wageni na kuchangia ukuaji wa sekta ya afya pamoja na mapato ya utalii visiwani humo.
Mpango huo ulioanza kutekelezwa rasmi Oktoba 1, 2024, unawataka wageni wote wa kimataifa wanaoingia Zanzibar kuwa na bima ya usafiri kabla ya kuwasili. Tangu kuanzishwa kwake, mpango huo umeendelea kuwa chanzo muhimu cha mapato, ukiingiza wastani wa dola za Marekani milioni moja, sawa na zaidi ya Sh bilioni 2.6 kila mwezi.
Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kwenye viwanja vya Magereza jijini Arusha, Ofisa Mauzo wa shirika hilo, Abdul-Halim Muhammad, alisema maonesho hayo yamewapa fursa ya kutoa elimu kwa watalii, wawekezaji na wadau wa sekta ya utalii kuhusu umuhimu wa bima hiyo.
NA MWANDISHI WETU – SONGEA
Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki maghala ya kuifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hii kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,
Ambao umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga
Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.

Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.
‘Mkoa hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.
Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.



Na Mwandishi Wetu
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amewashauri Waandishi wa Habari nchini kuipa thamani na heshima taaluma ya habari kwa kuzingatia nadhifu ya mavazi na mienendo yao wanapotekeleza majukumu ya kitaaluma.
Wakili Kipangula ametoa ushauri huo leo Juni 5, 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu “Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Enzi ya Kidijiti: Wajibu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari” kwenye Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari.
Amesema uandishi wa habari ni taaluma muhimu inayotambulika kama muhimili wa nne usio rasmi katika jamii, hivyo ni wajibu wa waandishi wenyewe kuhakikisha wanaijengea heshima kupitia mwenendo, maadili na namna wanavyojiwasilisha mbele ya jamii.
Wakili Kipangula amesema mwonekano wa mwandishi wa habari unaweza kuwa sehemu ya kujenga imani kwa jamii na vyanzo vya habari vinavyotoa taarifa mbalimbali kwa vyombo vya habari.
“Kwa hiyo hata mtu unavyoenda kumhoji mtu akikuona jinsi ulivyo anajua huyu mtu ataeleza kitu cha msingi na huyu mtu anaeleweka na ni wa maana,” amesema Wakili Kipangula.
Amesisitiza kuwa pamoja na kuzingatia maadili, sheria na weledi katika ukusanyaji na uchakataji wa habari, Waandishi wa Habari wanapaswa kutambua kuwa taswira wanayoijenga mbele ya jamii ni sehemu muhimu ya kuimarisha hadhi ya taaluma hiyo na kuongeza imani ya wananchi kwa vyombo vya habari.



Kongamano hilo liliwakutanisha wanafunzi wa shule za sekondari na vyuo vikuu, taasisi mbalimbali za Serikali, sekta binafsi pamoja na wadau wa maendeleo. Tukio hilo limefanyika ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.
Maadhimisho ya mwaka huu nchini yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Dira 2050: Tuwajibike Kupigania Tanzania,” inayolenga kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda mazingira na kuhakikisha maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Pia kuunganisha juhudi za Bunge, Serikali na wadau wengine katika kupinga unyanyapaa,



