Vodacom Foundation yatoa msaada wa vifaa vya elimu Kisarawe

Mwanafunzi wa darasa la sita Jonson Khamsini (wa pili toka kushoto) wa shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani akipokea vifaa vya elimu-madaftari,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set) pamoja na kalamu toka kwa Kaimu Ofisa Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia(kulia) ikiwa ni msaada ulitolewa na kampuni hiyo kupitia taasisi ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
Kaimu Ofisa Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia(kulia)akimkabidhi Mariam Yusuf msaada wa vifaa vya elimu,madaftari,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set)ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani.Msaada huo ulitolewa na kampuni hiyo kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani,wakigawiwa vifaa vya elimu na Kaimu Ofisa Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia(kulia) vikiwemo,madaftari,kalamu,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set) ikiwa ni msaada uliotolewa na kampuni hiyo kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
Meneja Biashara wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano cha Vodacom Tanzania, Grace Lyon (kulia) akiwagawia vifaa vya elimu wanafunzi wa shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani, vifaa walivyokabidhiwa ni,madaftari,kalamu,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set) ikiwa ni msaada uliotolewa na kampuni hiyo kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani,wakifurahia na kuviinua juu vifaa vyao vya elimu, Vikiwemo,madaftari,kalamu,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set) ikiwa ni msaada uliotolewa na Vodacom Tanzania kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
Wanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Chazige A iliyopo wilayani Kisarawe mkoani Pwani,Jonas Mkwagi (kushoto) na Khamis Haji(kulia) wakishirikiana na Meneja wa Vodacom Foundation,Sandra Oswald (katikati) kubeba boksi lenye vifaa vya elimu vikiwemo madaftari,kalamu,Mikebe yenye vifaa vya kusomea somo la hisabati (Mathematics set) ikiwa ni msaada uliotolewa na Vodacom Tanzania kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya jamii ya Vodacom Foundation hivi karibuni.
SHARE
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment