Zantel yakabidhi msaada kwa watoto wenye ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui Unguja.

Kampuni ya simu ya Zantel leo imekabidhi vifaa vya kusomea kwa watoto wenye vifaa vya ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui Unguja vyenye thamani ya shilingi milioni 20. Vifaa hivyo ni mashine ya perkins brailler, index printer, braillon paper pamoja na salte na stylus.

Msaada huo umekabidhiwa na Mshauri wa Mahusiano ya Umma wa Zantel, Mohamed Mussa kwa mwalimu mkuu wa shule Bi Taifa Ahmed pamoja na Mkurugenzi wa Elimu ya Shule ya Msingi, bwana Ahmed Abulmajid Shaaban.Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mohamed Mussa alisema vifaa hivyo ni sehemu ya mkakati wa  kampuni ya Zantel katika  kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata elimu bora bila kujali tofauti zao.

‘Wajibu wetu kama wanajamii ni kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapata msaada kama ilivyo kwa watu wengine na pia kuweza kuwaanda  kwa ajili ya kuweza kufikia malengo yao kama walivyo kusudia’ alisema Mussa. Shule ya msingi Kisiwandui ilianzishwa mwaka 1991, na mpaka sasa wanafunzi 199 wamepitia shuleni hapo.
 Mshauri wa Mahusiano ya Umma wa Zantel, Mohamed Mussa akizungumza wakati akikabidhi vifaa vya kusomea kwa watoto wenye ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui. kwa mwalimu mkuu wa shule Bi Taifa Ahmed pamoja na Mkurugenzi wa Elimu ya Shule ya Msingi, bwana Ahmed Abulmajid Shaaban. 
Mshauri wa Mahusiano ya Umma wa Zantel, Mohamed Mussa akikabidhi vifaa vya kusomea kwa watoto wenye ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui kwa Mkurugenzi wa Elimu ya Shule ya Msingi, bwana Ahmed Abulmajid Shaaban. Anayetazama katikati ni mwalimu mkuu wa shule Bi Taifa Ahmed. 
 Mshauri wa Mahusiano ya Umma wa Zantel, Mohamed Mussa akizungumza wakati akikabidhi vifaa vya kusomea kwa watoto wenye ulemavu wa macho wa shule ya msingi Kisiwandui. kwa mwalimu mkuu wa shule Bi Taifa Ahmed pamoja na Mkurugenzi wa Elimu ya Shule ya Msingi, bwana Ahmed Abulmajid Shaaban.
SHARE
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment