Teresia
Mhagama na Zuena Msuya.
Imeelezwa
kuwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China itatoa ufadhili wa masomo kwa
watanzania ili kujifunza masuala ya
makaa ya mawe kupitia Vyuo mbalimbali vya nchi hiyo ili kuongeza idadi ya wataalam hao nchini.
Hayo
yameelezwa jijini Dar es Salaam na Balozi China nchini Tanzania Dkt.Lu Youqing
wakati wa kikao chake na Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kilicholenga katika kujadili
uendelezaji wa makaa mawe nchini ambayo ni moja ya chanzo cha uzalishaji umeme.
Katika
kikao hicho Dkt. Youqing aliambatana na watendaji wa Serikali na kampuni mbalimbali zinazojishughulisha na
uendelezaji wa makaa ya mawe ikiwemo
kuzalisha umeme katika Jimbo linalojitegemea la Ningxia ambalo lipo nchini
China.
“
Mwaka ujao tutatoa ufadhili wa masomo kwa watanzania 10 hadi 15 kujifunza
masuala ya makaa ya mawe nchini China pia tutatoa ufadhili wa mafunzo ya muda
mfupi kwa wataalam waliopo kazini na Serikali ya Watu wa China itagharamia kila
kitu,” alisema Dkt. Lu Youqing.
Balozi
huyo wa China alisema hayo baada ya Profesa Muhongo kumueleza kuwa nchi ina
uhaba wa wataalam waliobobea katika masuala ya makaa ya mawe kwani hadi sasa
yupo mtaalam mbobezi mmoja ambaye naye anakaribia kustaafu.
“Tulikuwa
na mtaalam ambaye amekwishastaafu na sasa tumebakiwa na mmoja katika Wakala wa
Jiolojia Tanzania, hivyo ombi langu kuu ni kuendeleza watanzania katika sekta
hiyo ili tuwe na wataalam wa kutosha,
hivyo mwakani naomba mtusaidie kuwasomesha watanzania 10 hadi 20 na pia kutoa mafuzo ya muda mfupi
kwa wahandisi na wajiolojia ambao tayari wapo kazini,” alisema Profesa Muhongo.
Aidha
Profesa Muhongo alimsisitiza Balozi wa China nchini kuhakikisha kuwa maombi
hayo ya mafunzo ya makaa ya mawe hayaathiri
nafasi 20 za Ufadhili wa masomo ya Shahada za Uzamili na Uzamivu katika Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi ambazo
Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imepanga kutoa.
Akizungumzia
mashirikiano yanayoweza kufanyika kati ya Serikali ya Tanzania na Jimbo la
Ningxia, Profesa Muhongo aliwakaribisha watendaji wa Serikali hiyo na makampuni
ya nchi hiyo kushirikiana na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) ili kuiwezesha
maabara ya Wakala huo kuwa yenye teknolojia ya kisasa itakayowezesha kutambua
aina ya makaa ya mawe yaliyopo nchini pamoja na kuwa na takwimu sahihi za
mashapo ya madini hayo.
“
Takwimu za mashapo ya makaa ya mawe tunazozitoa sasa zimekuwa za kukadiria
hivyo tunahitaji mshirikiane na GST kushughulikia suala hilo ili tuwe na
takwimu sahihi za madini hayo,” alisema Profesa Muhongo.
Suala
lingine alilosisitiza kwa makampuni hayo ya
Ningxia ni kuwekeza katika uendelezaji wa mgodi wa makaa ya mawe wa
Kiwira ambapo mashapo yaliyopo katika mgodi huo yanaweza kuzalisha umeme wa
kiasi cha megawati 200 hadi 300 na kueleza kuwa Serikali haitatoa mgodi huo kwa
kampuni zisizokuwa na fedha wala teknolojia ambazo zinataka kuutumia mgodi huo
kupata fedha kwa mahitaji binafsi ya kampuni hizo.
Kwa
upande wake Mwakilishi Mkuu wa Masuala ya Uchumi na Biashara kutoka Jimbo la
Ningxia, Li Zighong, alisema kuwa Serikali ya Jimbo hilo imeamua kuwa na
Ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika uendelezaji wa makaa ya mawe kwani
Tanzania ni moja ya nchi barani Afrika ambayo ina sera nzuri zinazoongoza sekta
mbalimbali na hivyo kupelekea ukuaji wa
kiuchumi na kiteknolojia.
Alisema
kuwa Jimbo hilo la Ningxia linashika nafasi ya 6 nchini China kwa kuwa na wingi
wa mashapo ya makaa ya mawe na wana uzoefu wa uzalishaji umeme unaotokana na
nishati hiyo.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiwa na Mwakilishi Mkuu
wa Masuala ya Uchumi na Biashara kutoka Jimbo linalojitegemea la Ningxia nchini
China, Li Zighong (kushoto) katika mkutano uliolenga kuendeleza madini ya makaa ya mawe nchini ili
yaweze kuzalisha nishati ya umeme.Kikao kilifanyika katika Makao Makuu ya
Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar
es Salaam.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiwa na Mwakilishi Mkuu
wa Masuala ya Uchumi na Biashara kutoka Jimbo linalojitegemea la Ningxia nchini
China, Li Zighong (anayetia saini)
pamoja na Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania,
Dkt.Lu Youqing mara baada ya kumaliza mkutano uliolenga kuendeleza madini ya
makaa ya mawe nchini.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( katikati) akiongoza kikao
kilichojumuisha watendaji wa makampuni yanayojighulisha na Makaa ya Mawe
kutoka Jimbo linalojitegemea la Ningxia nchini China, Watendaji wa
Ubalozi wa Serikali ya Jamhuri ya Watu
wa China nchini Tanzania, na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na
Taasisi zake. Kikao hicho kililenga kujadili masuala mbalimbali ikiwemo
uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe yaliyopo nchini. Kushoto kwa Waziri ni
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa
James Mdoe na kulia kwa Waziri ni Mwakilishi Mkuu wa Masuala ya Uchumi na
Biashara kutoka Jimbo linalojitegemea la Ningxia nchini China, Li Zighong.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Wa Pili kulia) akiwa na
Mwakilishi Mkuu wa Masuala ya Uchumi na Biashara kutoka Jimbo linalojitegemea
la Ningxia nchini China, Li Zighong (wa
Pili kushoto) pamoja na Balozi wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China nchini
Tanzania, Dkt.Lu Youqing (wa kwanza kulia) wakiwa wameshikilia picha yenye
ujumbe wa kuusifu ushirikiano mzuri uliopo baina ya Serikali za Tanzania na
Jamhuri ya Watu wa China ambayo waliikabidhi kwa Profesa Muhongo mara baada ya
kumaliza mkutano uliolenga kuendeleza madini ya makaa ya mawe nchini ili yaweze
kuzalisha nishati ya umeme.
0 comments:
Post a Comment