


Na Mwandishi Wetu, Arusha.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika banda lao kwenye Maonyesho ya 31 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Themi Njiro jijini Arusha, ili kupata elimu kuhusu matumizi ya nishati safi na huduma nyingine muhimu zinazodhibitiwa na mamlaka hiyo.
Wito huo umetolewa na Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa EWURA, Mhandisi Lorivii Long'idu, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, ambapo alieleza kuwa EWURA inatumia maonyesho hayo kama jukwaa la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, hususan katika sekta za mafuta, umeme, gesi, na maji.
“Tunatumia fursa hii kusisitiza matumizi ya nishati safi siyo tu kwa ajili ya kulinda afya ya jamii, bali pia kwa kulinda mazingira,” alisema Mhandisi Long’idu, akisisitiza kuwa tafiti mbalimbali, ikiwemo zile kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), zimebaini kuwa magonjwa mengi ya mfumo wa upumuaji yanatokana na matumizi ya kuni na mkaa majumbani.
Mhandisi Long'idu alibainisha kuwa EWURA ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa miaka 10 wa Serikali unaolenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034, angalau asilimia 30 ya Watanzania watakuwa wanatumia nishati safi kama gesi, badala ya kuni na mkaa.
Aidha, aliongeza kuwa EWURA inasimamia kwa karibu ubora na usambazaji wa gesi, kuhakikisha kuwa wananchi wanapata bidhaa yenye ujazo sahihi. Alisema baadhi ya mawakala wasio waaminifu tayari wamechukuliwa hatua za kisheria na kesi zao zipo mahakamani.
“Ni jukumu la kila msambazaji mkubwa kuhakikisha kuwa wauzaji wadogo wanafuata sheria. Wananchi nao wanapaswa kuhakiki kuwa gesi wanayonunua imejaa kikamilifu na kupimwa vizuri,” alieleza.
Sambamba na hilo, alitoa wito kwa wananchi kufika kwenye banda la EWURA kujifunza zaidi kuhusu huduma zinazotolewa na mamlaka hiyo, pamoja na kutoa taarifa au malalamiko kuhusu changamoto mbalimbali wanazokutana nazo kwenye huduma za umeme, maji, mafuta na gesi ili zitafutiwe suluhisho.
Msaidizi wa Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Hotuba, Dkt. Cosmas Mwaisobwa, amekabidhiwa rasmi Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Presscard) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), leo tarehe 5 Agosti, 2025, baada ya kukidhi vigezo vya kisheria vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016.
Kitambulisho hicho kimetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dodoma.
Dkt. Mwaisobwa, ambaye ni miongoni mwa wataalamu wachache nchini wenye shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika Mawasiliano kwa Umma na Uandishi wa Habari, ameungana na Dkt. Egbert Mkoko (Mjumbe wa Bodi) na Dkt. Ayoub Chacha Rioba (Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania – TBC), waliomtangulia kupokea vitambulisho hivyo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi kitambulisho hicho, Wakili Kipangula alimpongeza Dkt. Mwaisobwa kwa kutekeleza matakwa ya kisheria na kuwasihi waandishi wengine kufuata mfano huo kwa ajili ya kuhalalisha shughuli zao za kihabari.
“Tunaendelea kuwahimiza waandishi wote nchini kuhakikisha wanakamilisha usajili na kupata Ithibati na Vitambulisho kwa mujibu wa sheria, ili waweze kutekeleza majukumu yao bila changamoto za kisheria,” alisema Kipangula.
Kuhusu mwenendo wa maombi ya Ithibati, Wakili Kipangula alisema kuwa hadi kufikia tarehe 5 Agosti 2025, Bodi imepokea jumla ya maombi 3,200 ambapo 2,109 yameidhinishwa, 674 bado yapo katika mchakato wa uchambuzi, huku maombi 43 yakikataliwa kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa.
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam.
Wakazi wa Kata ya Kinyerezi, Jijini Dar es Salaam, wametangaziwa kurejea kwa huduma ya majisafi mapema leo, Agosti 4, 2025, kufuatia kukamilika kwa matengenezo ya bomba la usambazaji maji lililoathiri maeneo mengi ya kata hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mhandisi wa Usambazaji Maji kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), Antony Budaga, amesema matengenezo hayo yamehusisha ubadilishaji wa kipande cha bomba la inchi 12 kwa umbali wa takribani mita 310, kwa lengo la kuboresha huduma ya maji kwa wakazi wa Kinyerezi.
Maeneo yanayotarajiwa kurejea kwa huduma ni pamoja na Sabasaba, Stakishari, Mongo la Ndege Shule ya Msingi, Mpera, Mwembeni, Mnembwe kwa Balozi Vick, Zimbili A (Darajani), St. Rosalia, Zimbili kwa Balozi, Serikali ya Mtaa Zimbili, Kwa Diwani Leah, Mwaipaya, Mnembwe, Garage ya Wachina, Mnara wa Voda, Kwa Smart, Kwa Makadali, NSSF Kota, Mbuyuni, Saloon Mafuta ya Taa, Ngekili, Msikitini, Shule ya Msingi Kinyerezi, Kanga Chini, Mtaa wa Uzinguni, Machinjio ya Nguruwe, Kwa Kipofo, Kanisa la Wasabato Kanga Chini, Kwa Angles, Mtaa wa Kwa Tozi, Maduka Saba, New Vibe, Michael Mausa, BL Park, Kinyerezi Park, Flamingo, Njombe Road, Zimbili Msikitini wa Njano, Kwa Simba Chawene na Kwa Msemwa.
DAWASA imewahakikishia wakazi wa maeneo hayo kuwa huduma itaendelea kuimarika kadri kazi ya uunganishaji wa bomba jipya inavyokamilika.
Na Mwandishi Wetu, Arusha.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na Wahariri wa Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025.
Kibaha, Julai 30, 2025: Katika uchaguzi wa ndani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika leo katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kwamfipa – Kibaha Mjini, wagombea Hawa Mchafu Chakoma na Mariam Ibrahim wameibuka vinara katika nafasi ya Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani.