Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad akiwa na Mwenyeji wake, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela, wakisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Shuleni hapo tayari kwa uzinduzi rasmi.
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela, wakiangalia umahiri wa Mtoto Martha katika kutaja mikoa ya Tanzania aliyokuwa akiitaja kwa kuonyesha ramani.
---
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad, amefanya ziara ya siku 2 Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Kilolo na Wilaya ya Iringa na kufanya shughuli ya kuzindua shule ya watoto ya awali inayofundisha mwa mfumo wa Montesori.
---
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad, amefanya ziara ya siku 2 Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Kilolo na Wilaya ya Iringa na kufanya shughuli ya kuzindua shule ya watoto ya awali inayofundisha mwa mfumo wa Montesori.
Shule
hiyo iliyopo Ilula, katika wilaya ya Kilolo inafadhiriwa na wanachi wa
Norway kupitia kwa mdau wa Maendeleo Norway na familia yake Bw. Osmund
pamoja na wananchi wengine ambao wameunda NGO iitwayo Ilula Orphanage
Program (IOP) chini ya Mwenyekiti wake raia wa Marekeni Bibi Berit
Skaare.
Akimkaribisha
Balozi kuzindua Shule hiyo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye ni Mkuu
wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela, alisifu na kushukuru wananchi wa
Norway kwa kazi kubwa wanayofanya Tanzania hasa katika elimu, Pia
alipongeza juhudi za wananchi wa Norway wanavyo jali watanzania.
Kasesela
aliagiza Halmashauri kutunza kituo hicho na kuhakikisha kinaendelea
kuwa bora na kufundisha watoto wetu, Pia aliagiza Halmashauri iangalie
uwezekano wa kutengeneza barabara ya kufika kituoni hapo kwani kwa sasa
hairidhishi.
Nae
Balozi wa Norway nchini, Hanne Marie, alishukuru serikali ya Tanzania
na kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kasi anayokwenda nayo
kukomboa elimu. Pia alishukuru Mkoa wa Iringa kwa kutoa ardhi ili
ijengwe shule hiyo ya kisasa. Balozi aliaahidi kuendeleza ushirikiano na
Tanzania katika nyanja ya elimu hasa elimu ya ufundi stadi.
Balozi
aliendelea na ziara yake kukagua miradi ya REA ambayo baadhi
inafadhiliwa na serikali ya Norway. Atatembelea mradi wa Mgama ulioko
kata ya Lumuli Iringa.
0 comments:
Post a Comment