CHUO KIKUU ARDHI CHAWAPA MWONGOZO WANAFUNZI WA SHULE ZA SEKONDARI ZA JIJI LA DAR ES SALAAM KUHUSU NAMNA BORA YA KUJIUNGA NA MASOMO YA ELIMU YA JUU KULINGANA NA UFAULU WAO JUU


Mtaalam wa Jiografia kutoka Chuo Kikuu Ardhi Dkt. Mlenge Fanuel Mgendi  akiwahamasisha wanafunzi wa kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani  kupenda kusoma na kuweka bidii katika masomo ambayo wana uwezo nayo ili yawasaidie kuendelea na Elimu ya Juu katika chuo Kikuu Ardhi na vyuo vingine leo jijini Dar es salaam. Chuo Kikuu Ardhi kinaendesha Programu ya utoaji elimu kwa wanafunzi wa sekondari katika shule mbalimbali kwa lengo la kuwasaidia  kufanya uchaguzi sahihi wa kozi za masomo wanazotarajia kuendelea nazo pindi watakapohitimu masomo ya elimu ya Sekondari.
SHARE
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment